Wednesday, August 22, 2012

SANTOS AKABILIWA NA KIFUNGO KWA KUENDESHA MWENDO KASI.

MCHEZAJI nyota wa klabu ya Arsenal Andre Santos huenda akakabiliwa na adhabu ya kifungo jela baada ya polisi kumtuhumu kukimbiza gari lake kwa spidi kubwa inayofikia kilometa 130 kwa saa. Beki huyo wa kimataifa wa Brazil alifanya tukio hilo wakati akielekea mazoezini kwenye klabu yake hiyo ambapo alikuwa gari lake la kifahari aina ya Maserati GranTurismo alilonunua kwa paundi 110,000. Polisi wanadai kuwa mchezaji huyo alipita kwa mwendo kasi huo na kuwakimbia polisi ambapo anaweza kufungwa jela kama akipatikana na hatia ya kuendesha mwendo wa hatari. Polisi waliendelea kudai kuwa walimsimamisha mchezaji huyo lakini hakusikia lakini alifanikiwa kumsimamisha akiwa amekaribia kabisa sehemu ya kufanyia mazoezi ya klabu yake umbali wa mita 500.

No comments:

Post a Comment