Wednesday, August 22, 2012

SIX AFURAHISHWA NA KUREJEA KWA ADEBAYOR KATIKA KIKOSI CHA TOGO.

KOCHA wa timu ya taifa ya Togo, Didier Six amewaambia waandishi wa habari jijini Lome kuwa amefurahishwa na kitendo cha mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Emmanuel Adebayor kurejea katika kikosi chake baada ya kukataa kufanya hivyo kwa kipindi kirefu. Six aliendelea kusema kuwa Adebayor mwenye umri wa miaka 28 alimfuata wakati akiwa mapumzikoni ambapo Togo ilikuwa ikicheza mchezo wa kirafiki na Burkina Faso nchini Ufaransa na kumuomba ampange katika kipindi cha pili. Ingawa walipoteza mchezo huo kwa mabao 3-0 lakini kocha huyo amesema kuwa alifarijika na kiwango pamoja na morali waliyoonyesha wachezaji wake pindi Adebayor alipoingia uwanjani. Kocha huyo amesema kuwa kikosi chake kina morali ya kutosha tayari kwa mchezo wa kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika 2013 dhidi ya Gabon na lazima atamjumuisha Adebayor katika kikosi chake hicho. Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester City ambaye amehamia moja kwa moja katika klabu ya Tottenham Hotspurs alipokuwa akicheza kw mkopo alikataa kuichezea timu ya taifa ili kuwashinikiza viongozi wa soka nchini kwake kuwahakikishia wachezaji wa timu hiyo usalama, usafiri wenye uhakika na malazi bora.

No comments:

Post a Comment