Wednesday, August 22, 2012

SENEGAL YATAKA MCHEZO BAINA YAO NA IVORY COAST UCHEZWE NEUTRAL GROUND KUTOKANA NA MACHAFUKO JIJINI ABIDJAN.

KUFUATIA matukio ya kivita yanaoendelea nchini Ivory Coast, Shirikisho la Soka la Senegal-FSF limesema kuwa linaweza kuomba kubadilishiwa eneo la mchezo wa kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika 2013 ambao ulikuwa uchezwe jijini Abidjan Septemba 8 mwaka huu. Rais wa FSF, Augustin Senghor amesema kuwa kutokana na hali ilivyo nchini Ivory Coast atalazimika kuomba Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF kuhamishia mchezo huo katika nchi yoyote jirani kwa ajili ya usalama wa wachezaji wake. Senghor aliendelea kusema kuwa hata CAF wenyewe hawataweza kukubali mchezo huo kuchezwa jijini Abidjan ambapo kuna matukio ya kurushiana risasi yanayoweza kuathiri wachezaji wakati wa mchezo baina ya timu hizo. Watu wasiojulikana waliokuwa na silaha walianzisha mapigano jijini humo wiki mbili zilizopita dhidi ya kambi za kijeshi, vituo vya polisi na kwenye vizuizi katika mji huo na kusababisha vifi vya watu wapatao 15 na pia kufunja magereza na kuwaachia wafungwa waliokuwemo ndani. Hatahivyo Wizara ya Ulinzi nchini Ivory Coast imewahakikishia wananchi kuwa wamefanikio kudhibiti tukio hilo na wameweka askari wa kutosha ili kulinda eneo ilipotokea machafuko hayo.

No comments:

Post a Comment