Thursday, August 23, 2012

BOLT, BLAKE KUKUTANA DIAMOND LEAGUE, USWIS.

BAADA ya kumalizika kwa michuano ya Olimpiki iliyofanyika jijini London, wanariadha walioshiriki michuano hiyo duniani kote wanakutana tena baadae usiku michuano ya Diamond League itakayofanyika nchini Switzerland.
Mkimbiaji nyota wa mbio fupi Usain Bolt anatarajiwa kukimbia mbio za mita 200 zitakazofanyika jijini Lausanne, lakini ni kama anakuwa anamkwepa Mjamaica mwenzake Yohan Blake ambaye atakimbia mbio za mita 100. Katika michuano ya olimpiki nyota hao walishiriki mbio zote mbili za mita 100 na 200 kwa pamoja ambapo Bolt alishinda zote kabla ya kuunganisha nguvu kwa pamoja na kukimbia mbio za kupokezana vijiti za mita 400 na kuvunja rekodi ya dunia. Akihojiwa Blake amesema kuwa anapenda kukimbia kushindana na Bolt lakini inabidi uamuzi huo amuachie meneja wake kwakuwa yeye ndiye anafahamu anachokifanya. Wawili hao pia hawatakutana katika katika michuano ya Diamond League itakayofanyika jijini Zurich na Brussels kabla ya kumaliza msimu wao.

No comments:

Post a Comment