Wednesday, August 29, 2012

LAMPARD ATAKA KUINOA CHELSEA.

KIUNGO nyota wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Chelsea, Frank Lampard amesema kuwa anataka kuwa kocha wa klabu hiyo ambao ndio mabingwa wa vilabu barani Ulaya wakati atakapomaliza kipindi chake cha kucheza soka. Lampard ambaye ana umri wa miaka 34 amekuwa akicheza katika Ligi Kuu nchini Uingereza toka mwaka 2001 na hivi sasa yuko katika msimu wake wa mwisho katika mkataba wake. Akihojiwa kuhusu suala la mkataba wake Lampard amesema anachofikiri sasa ni kutafuta leseni ya ukocha lakini ni klabu moja tu ambayo angependa kufundisha nayo ni Chelsea. Lampard amesema anajua kuwa kauli yake hiyo inaweza kupondwa na wadau wengine wa mchezo wa soka lakini yeye hataki kuanzia kufundisha katika vilabu vidogo kama wengine. Kiungo huyo alikuwa nahodha wakati wa mchezo wa fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich na kukiongoza vyema kikosi hicho kunyakuwa taji lake la kwanza la michuano hiyo pamoja lile la FA.

No comments:

Post a Comment