Tuesday, August 28, 2012

OFISA ACHOMWA NA MKUKI KOONI KATIKA MASHINDANO HUKO UJERUMANI.

OFISA mmoja katika michuano ya riadha iliyokuwa ikifanyika jijini Dusseldorf nchini Ujerumani amefariki dunia baada ya kuchomwa na mkuki katika koo wakati michuano hiyo ikiendelea. Ofisa huyo aliyejulikana kwa jina la Dieter Strack mwenye umri wa miaka 74 alikimbizwa hospitali mara baada ya tukio hilo lakini alifariki baadae kutokana na majeraha hayo. Taarifa kutoka vyombo vya habari vya nchi hiyo zinasema kwamba Strack alikumbwa na tukio hilo wakati akikimbia kwenda kupima umbali utakapotua mkuki uliotupwa lakini kabla ya mkuki huo kufika chini ulitua katika koo lake na kumjeruhi vibaya. Msemaji wa polisi katika mji huo Andre Hartwig amesema kijana aliyerusha mkuki huo ulioleta maafa ambaye ana umri wa miaka 15 alipelekwa kliniki ambako anapewa ushauri nafasa kutokana na tukio hilo. Matukio kama hayo katika michuano ya riadha hususani mchezo wa kurusha mkuki na kutupa tufe yamekuwa yakitokea lakini ni mara chache kusababisha kifo. Mwaka 2007 mwanariadha wa mbio za kuruka chini wa Ufaransa Salim Sdiri alichomwa na mkuki katika mashindano ya mchezo huo yaliyofanyika jijini Rome, Italia na kupelekwa hospitalini ambapo baadae alipona majeraha aliyopata.

No comments:

Post a Comment