Tuesday, August 28, 2012

CLIJSTERS AANZA VYEMA US OPEN.

MCHEZA tenisi nyota Kim Clijsters ameanza vyema michuano yake ya mwisho mikubwa kabla ya kustaafu baada ya kumfunga Victoria Duval kutoka Marekani katika mzunguko wa kwanza wa michuano ya wazi ya Marekani. Clijsters ambaye ni bingwa wa michuano hiyo mwaka 2005, 2009 na 2010 alifanikiwa kushinda mchezo wake huo wa kwanza kwa 6-3 6-1 dhidi ya Duval ambaye anachipukia katika mchezo huo akiwa umri wa miaka 16. Mwanamama huyo ambaye ni raia wa Ubelgiji sasa atakutana na Laura Robson raia wa Uingereza katika mzunguko wa pili wa michuano inayoendelea jijini New York Marekani. Mbali na Clijsters michezo mingine iliyochezwa jana bingwa mtetezi wa michuano hiyo Sam Stosur raia wa Australia amefanikiwa kusonga mbele baada ya kumfunga Petra Martic wa Urusi kwa 6-1 6-1. Maria Sharapova kutoka urusi ambaye ni bingwa wa michuano hiyo mwaka 2006 naye alifanikiwa kuzonga mbele baada ya kumfunga Melinda Czink kutoka Hungary kwa 6-2 6-2 wakati bingwa wa michuano ya wazi ya Australia Victoria Azarenka pia alishinda mchezo wake kwa 6-0 6-1 dhidi ya Alexandra Panova.

No comments:

Post a Comment