Monday, August 27, 2012

BRAZIL KUCHEZA NA URENO.

TIMU ya taifa ya Brazil inatarajiwa kucheza michezo miwili ya nyumbani na ugenini ya kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Ureno mapema mwaka 2013 ikiwa kama sehemu ya maandalizi ya Kombe la Dunia mwaka 2014 ambayo nchi hiyo itakuwa mwenyeji. Mchezo wa kwanza wa kirafiki baina ya timu hizo unatarajiwa kuchezwa jijini Sao Paulo huku wa pili ukichezwa nchini Ureno katika tarehe ambazo zitatangazwa hapo baadae. Mbali na michezo hiyo miwili maofisa wa soka wan chi hiyo wamesema kuwa timu hiyo pia imejipanga kucheza mchezo mwingine wa kimataifa wa kirafiki na timu ya taifa ya Uingereza. Kabla ya michezo hiyo Brazil inatarajiwa kucheza na timu ya taifa ya Afrika Kusini-Bafana Bafana Septemba 7 mwaka huu mchezo ambao utafanyika jijini Sao Paulo kabla ya kucheza na China jijini Racife siku tatu baadae.

No comments:

Post a Comment