Monday, August 27, 2012

PUYOL AUMIA TENA.

NAHODHA wa klabu ya Barcelona, Curles Puyol amevunjika mfupa wa mguu wake wa kulia wakati wa mchezo baina ya timu yake na Osasuna ambao walishinda mabao 2-1. Katika taarifa yake klabu hiyo imesema kuwa mchezaji huyo inabidi afanyiwe vipimo zaidi vya xray ili kujua ukubwa wa tatizo hilo na muda gani atakuwa nje ya uwanja. Puyol mwenye umri wa miaka 34 anatarajiwa kukosa mchezo muhimu wa Super Cup baina ya timu yake na mahasimu wao Real Madrid utakaofanyika katika Uwanja wa Santiago Bernabeu Alhamisi ya wiki hii, ukiwa ni mchezo wa pili baada ya ule wa kwanza Barcelona kuibuka na ushindi wa mabao 3-2. Mchezaji huyo aliumia katika dakika za majeruhi katika Uwanja wa Reyno de Navarra baada ya kugongana na mchezaji wa Osasuna Roland Lamah wakati akiwa katika harakati za kumzuia. Katika kipindi cha misumu ya hivi karibuni Puyol amekuwa akindamwa na majeruhi ya mara kwa mara ukiwemo upasuaji mguu wake wa kulia aliofanyiwa na kusababisha kushindwa kuichezea Hispania katika michuano ya Ulaya.

No comments:

Post a Comment