Monday, August 27, 2012

MADRID YANYAKUWA RASMI MODRIC.

KLABU ya Tottenham Hotspurs ya Uingereza imefikia makubaliano na klabu ya Real Madrid juu ya uhamisho wa mchezaji wake Luka Modric kwa ada ya paundi milioni 30. Kiungo huyo wa kimataifa kutoka Croatia mwenye miaka 26 anatarajiwa kusafiri kuelekea Hispania kwa ajili kufanyiwa vipimo vya afya kabla ya kusainishwa mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo. Tottenham pia katika taarifa yake iliyotuma katika mtandao wake wamesema kuwa mbali na kukubali kumuuza mchezaji huyo pia klabu hiyo imetangaza kuingia ubia na Madrid ambapo katika makubaliano ya ubio huo klabu hizo zitakuwa zikibadilishana mafunzo pamoja na uhusiano wa kibiashara. Mwenyekiti wa Tottenham, Daniel Levy amesema kuwa Modric amekuwa mchezaji wao kutegemewa na walikuwa hawahitaji kumuachia lakini wamefarijika kwamba amekwenda Madrid klabu ambayo katika siku mbeleni watakuwa na mahusiano nao mazuri kwa ajili ya maendeleo. Modric alijiunga na Tottenham mwaka 2008 kwa ada ya paundi milioni 16.5 akitokea klabu ya Dinamo Zagreb ya nchini kwake ambapo mpaka anaondoka amefunga mabao 17 katika michezo 150 aliyocheza katika timu hiyo.

No comments:

Post a Comment