Monday, August 27, 2012

CLIJSTERS ATARAJI KUSTAAFU TENISI NA TAJI LA US OPEN.

MCHEZAJI tenisi nyota ambaye ni bingwa mara tatu wa michuano ya wazi ya Marekani au US Open, Kim Clijsters anatarajia kustaafu mchezo huo kwa kushinda michuano hiyo ambayo imeanza leo jijini New York. Clijsters ambaye ana umri wa miaka 29 alitangaza nia yake ya kustaafu mchezo huo mara baada ya michuano ya US Open na amekuwa katika ziara ya kuaga katika kipindi chote cha msimu huu. Majeraha yaliyikuwa yakimkabili yalimzuia mchezaji kushiriki michuano mingi msimu huu lakini amesema kuwa hivi anajiamini na yuko vyema kwa ajili ya kutetea taji la michuano hiyo ambalo alilichukua mwaka jana. Clijsters alishindwa kutamba katika michuano ya michuano ya olimpiki iliyofanyika jijini London baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Maria Sharapova katika mchezo wa robo fainali ya michuano hiyo. Mara ya kwanza Clijsters alitangaza kustaafu mchezo huo mwaka 2007 baada ya kusumbuliwa na majeraha ya muda mrefu lakini alibadilisha mawazo miaka miwili baadae na kurejea uwanjani na kushinda michuano ya US Open kabla ya kufanya hivyo tena mwaka 2010 na 2011.

No comments:

Post a Comment