Thursday, August 30, 2012

RATIBA YA MAKUNDI UEFA CHAMPIONS LEAGUE KUPANGWA LEO.

KLABU ya Manchester City huenda ikapangwa kundi moja na timu za Ujerumani, Hispania na Italia katika ratiba ya makundi ya michuano ya Klabu Bingwa ya Ulaya inayotarajiwa kufanyika baadae leo. Mabingwa wa Ligi Kuu nchini Uingereza, City ambao walitolewa katika hatua ya makundi msimu uliopita wamewekwa katika chungu cha pili katika upangaji wa ratiba hizo na kuna uwezekano wakakutana na timu za Borussia Dortmund, Real Madrid na Juventus. Mabingwa watetezi wa michuano hiyo Chelsea, Arsenal na Manchester United wenyewe watakuwa katika chungu cha kwanza katika uapngaji wa ratiba ya michuano hiyo. Ratiba hiyo itajumuisha timu 32 ambazo zitagawanywa katika vyungu vinne ambavyo vitawagawanya katika makundi makundi nane yatakayokuwa na timu nne kila kundi. Michezo katika hatua makundi inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 18 na 19 na kumalizika Desemba 4 na 5.

No comments:

Post a Comment