Thursday, August 30, 2012

US OPEN: AZARENKA, SHARAPOVA WASONGA MBELE, CLIJSTERS NJE.

Laura Robson.
NYOTA wa tenisi wanaoongoza kwa ubora katika orodha ya wachezaji wanawake wa mchezo huo, Victoria Azarenka na Maria Sharapova wamefanikiwa kutinga katika mzunguko wa tatu wa michuano ya wazi ya Marekani inayojulikana kama US Open. Azarenka ambaye katika orodha hizo anashika namba moja alifanikiwa kumfunga Kirsten Flipkens kutoka Ubelgiji kwa 6-2 6-2 wakati Sharapova ambaye anashika namba mbili yeye alitumia muda wa dakika 54 kumchapa Lourdes Dominguez Lino kwa 6-0 6-1. Bingwa mtetezi wa michuano hiyo Sam Stour pia alifanikiwa kusonga mbele baada ya kumfunga Edina Gallovits-Hall wa Romania kwa 6-3 6-0 wakati wachezaji wengine nyota kama Petra Kvitova na Li na nao walisonga mbele baada ya kushinda katika michezo yao. Laura Robson kutoka uingereza alifanikiwa kupata ushindi wake wa kwanza mkubwa baada ya kumfunga mchezaji namba moja wa zamani Kim Clijsters katika mzunguko wa pili wa michuano hiyo. Clijsters alitarajia kushinda taji hilo kabla ya kustaafu mchezo huo kama alivyotangaza awali lakini alishindwa kutamba mbele ya kinda Robson ambaye ana umri wa miaka 18 kwa kufungwa kwa 7-6 7-6 wakitumia dakika 126.

No comments:

Post a Comment