Thursday, August 30, 2012

ROONEY AAPA KUBAKIA UNITED.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Manchester United, Wayne Rooney ameapa kubakia katika klabu hiyo na kuhakikisha anapambana ili kujihakikishia mstakabali wake katika kikosi hicho. Kuna tetesi zilizokuwa zimesambaa mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa kuna hali ya kutoelewana kati ya meneja wa United, Sir Alex Ferguson na mchezaji huyo wakati wakipindi cha kujiandaa kwa ajili ya msimu mpya wa ligi. Tetesi hizo ziliongezeka nguvu baada ya Ferguson kumuacha mchezaji huyo katika kikosi chake kilichocheza dhidi ya Fulham Jumamosi iliyopita na kuzua maswali mengi juu ya mstakabali wa mchezaji huyo katika siku za mbele. Lakini jana usiku mchezaji huyo alituma ujumbe katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kuwa anazisikia habari hizo kutoka kwa watu na kukanusha kwamba sio za kweli. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 26 atakuwa nje ya uwanja kwa miezi miwili baada ya kuumia wakati wa mchezo dhidi ya Fulham ambao aliingia kama mchezaji wa akiba. Ujio wa Robin van Persie ambaye ameajiliwa kutoka Arsenal kwa ada ya paundi milioni 22 unamaanisha kuwa Ferguson ana washambuliaji wa kutosha wakiwemo Danny Welbeck na Javier Hernandez hata kama Rooney akiamua kuondoka.

No comments:

Post a Comment