Thursday, August 30, 2012

ZAMALEK YAJIPANGA KUWALINDIA MASHABIKI WAKE HESHIMA PAMOJA NA KUTOLEWA CHAMPIONS LEAGUE.

Jorvan Vieira, Zamalek Coach.
KLABU kongwe ya soka nchini Misri, Zamalek inatarajiwa kuwa na mashabiki wake wakati watapoikaribisha timu ya Chelsea Berekum ya Ghana katika mchezo wa kundi A wa michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika utakachezwa Jumamosi. Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hiyo imekubali kuruhusu mashabiki kuhudhuria mchezo huo wa ligi ya mabingwa kwa mara ya kwanza baada ya miezi saba kupita. Mashindano yote ya soka ya ndani nchini humo yamesimamishwa kufuatia vurugu zilizotokea huko Port-Said Februari mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 74 na wengine mamia kujeruhiwa. Katika mchezo huo Zamalek hawatakuwa na nafasi ya kusonga mbele katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo lakini wataingia uwanjani ili kuwapa imani mashabiki wao baada ya kuwa na msimu usioridhisha kwenye ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment