Friday, August 31, 2012

VALCKE ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UJENZI WA VIWANJA BRAZIL.

KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Jerome valcke amesema kuwa maandalizi kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil yanaendelea vyema. Valcke amesema kuwa viwanja vyote vinajengwa kwa wakati huku miradi mingine nayo ikiendelea vizuri na kufikia kasi ambayo FIFA ilikuwa inahitaji ili viweze kukamilika kwa wakati. Kauli aliitoa baada ya kufanya ziara yake ya nne nchini humo kuangalia maendeleo ya maandalizi akipingana na kauli yake aliyoitoa Machi mwaka huu kuhusu maandalizi ya nchi hiyo na kuzua mtafaruku mkubwa na serikali ya nchi hiyo. Baadae valcke aliomba msamaha kuhusiana na kauli yake hiyo akidai watu walichukulia suala alilosema kwa ubaya kabla ya Rais wa FIFA kuomba radhi kuhusiana na suala hilo. Valcke alitembelea kuangalia maendeleo ya viwanja na miundo mbinu katika mji wa Manaus uliopo Kaskazini mwa nchi hiyo pamoja na mji wa Cuiaba ambao upo katikati mwa jimbo la Mato Grosso.

No comments:

Post a Comment