Friday, August 31, 2012

BOLT BLAKE WANG'ARA DIAMOND LEAGUE.

WANARIADHA nyota wa mbio fupi kutoka Jamaica, Usain Bolt na Yohane Blake wameendelea kung’aa katika msimu wa mwishoni wa michuano ya Diamond League baada ya kushinda katika mbio za mita 100 na 200. Wawili hao hawajakimbia pamoja toka walipofanya hivyo katika michuano ya Olimpiki, walikwepana tena katika mbio hizo baada ya Bolt kushinda za mita 200 akitumia muda wa sekunde 19.66 na Blake kushinda za mita 100 akitumia muda wa sekunde 9.76. Akiongea kabla ya mbio hizo Blake ambaye ni mshindi wa medali ya fedha katika michuano ya olimpiki alisema kuwa anategemea kushangaza watu tena katika mbio hizo lakini alishindwa kufanya hivyo kutokana na hali ya hewa ya mvua iliyokuwepo. Blake alishinda kirahisi mbio hizo baada ya mpinzani wake mkubwa Tyson Gay kutoka Marekani kuondolewa baada ya kuanza kuchomoka kabla ya wenzake. Mkenya David Rudisha ambaye alivunja rekodi yake mwenyewe ya dunia aliyoweka katika mbio za mita 800 katika michuano ya olimpiki alishindwa kutamba katika mbio hizo baada ya kupitwa wakati wakumalizia mbio hizo na Mohammed Aman kutoka Ethiopia.

No comments:

Post a Comment