Tuesday, August 21, 2012

WACHEZAJI HAMKUTUMIA VYEMA VAN PERSIE - FERGIE.

MENEJA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amesema kuwa kikosi chake kilishindwa kumtumia ipasavyo mshambuliaji nyota mpya wa klabu hiyo aliyesajiliwa hivi karibuni Robin van Persie. Bao la kichwa lililofungwa na Marouane Fellaini katika kipindi cha pili lilitosha kuipa ushindi Everton waliokuwa wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani dhidi ya United ambayo ilicheza bila kuwepo kwa mabeki wake wanne ambao ni majeruhi. Van Persie ambaye alisajiliwa na United kwa ada ya paundi milioni 24 aliingia akitokea benchi la wachezaji wa akiba katika kipindi cha pili lakini alishindwa kupata bao katika mchezo huo kama mashabiki wengi wa klabu hiyo walivyokuwa wakitegemea. Ferguson amesema kuwa tatizo kubwa la mchezaji kushindwa kufunga ni upande wa pembeni ambao alikuwa akimchezesha kwenye mchezo huo tofauti na ile nafasi ya katikati ambayo amezoea kucheza wakati akiwa Arsenal. Van Aliingia katika dakika ya 68 akichukua nafasi ya Danny Welbeck ambaye alianza katika mchezo huo lakini hakuweza kuiokoa timu hiyo kuepuka kipindi cha kwanza toka mwaka 2004 katika mchezo wa ufunguzi wa Ligi kuu nchini Uingereza.

No comments:

Post a Comment