Tuesday, August 21, 2012

PARDEW KUKUBALI KUFUNGIWA MECHI MBILI NA FA.

MENEJA wa klabu ya Newcastle United Alan Pardew hatopinga adhabu atakayopewa na Chama cha Soka nchini Uingereza-FA kwa kosa la kumsukuma mwamuzi msaidizi wakati wa mchezo baina ya timu yake na Tottenham Hotspurs ambao ulimaliza kwa ushindi wa mabao 2-1. Pardew alitolewa katika benchi la ufundi la klabu hiyo na kuamriwa kwenda kukaa jukwaani na mashabiki baada ya kumsukuma mshika kibendera Peter Kirkup wakati akidai mpira uliokuwa umetoka nje nakuamriwa kurushwa katika lango lao. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 51 amepewa muda wa mpaka alhamisi awe amekata rufani lakini hatahivyo inaaminika kuwa atakubali uamuzi utakaotolewa na FA uamuzi ambao unatarajiwa kuwa ya kufungiwa michezo miwili. Pardew aliomba radhi kwa mwamuzi wa mchezo huo Martin Atkinson na pia mbele ya vyombo vya habari kwa kitendo alichofanya lakini mwamuzi Atknson aliamua kutaja tukio hilo katika ripoti yake aliyowasilisha kuhusu mchezo huo.

No comments:

Post a Comment