Wednesday, August 29, 2012

WALCOTT ACHOMOA MKATABA MPYA.

MSHAMBULIAJI wa pembeni wa klabu ya Arsenal, Theo Walcott amekataa kusaini mkataba mpya na klabu hiyo lakini mazungumzo bado yanaendelea baina yake na klabu. Nyota huyo mwenye miaka 23 ambaye mkataba wake unatarajiwa kuisha mwaka 2013 bado anataka kubakia klabuni hapo kama watamboreshea maslahi yake. Matajiri wa jiji la Manchester klabu ya Manchester City wanatambua kinachoendelea juu ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza na wanaweza kujaribu kumyakuwa kama Arsenal wakishindwa kumpa mchezaji huyo anachotaka. Kuna taarifa kwamba Arsenal ambao wamempa mkataba utakaomuwezesha kulipwa paundi 75,000 kwa wiki mchezaji huyo kama wakishindwa kufikia makubaliano watamuuza mchezaji kabla ya kufingwa kwa dirisha la usajili Agosti 31. Kama mchezaji huyo akiondoka atakuwa ni mchezaji watatu wakutegemewa wa klabu hiyo kuondoka baada ya Robin van Persie aliyekwenda Manchester United na Alex Song aliyekwenda Barcelona.

No comments:

Post a Comment