Wednesday, August 29, 2012

BLATTER APINGA KUWEPO SHERIA YA UMRI WA KUGOMBEA FIFA.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter anapinga vikali kuwepo kwa sheria ya umri wa kiongozi anayetakiwa kuongoza shirikisho hilo ingawa anajiandaa kukubali uwepo wa ukomo wa uongozi. Blatter ambaye ana umri wa miaka 76 pia alipinga suala la viwanja vya soka kuwa na sehemu ya kusimama ambapo suala hilo lilimyuingiza katika mgongano na Ligi Kuu nchini Ujerumani maarufu kama Bungasliga ambayo baadhi ya viwanja vyake vina sehemu ya kusimama. Akihojiwa Blatter aliliambia gazeti moja la michezo nchini Ujerumani kuwa anaunga mkono suala la uongozi wa shirikisho hilo kuwa na ukomo lakini anapinga suala la watu wenye umri mkubwa kutopewa nafasi ya kugombea uongozi FIFA. Blatter amesema kuwa hadhani kama umri wa mtu ukiwa mkubwa ndio unamzuia kugombea nafasi za uongozi kwani wapo viongozi wengi wenye umri mkubwa lakini akli zao zinafanya kazi kama vijana. Bosi huyo wa FIFA pia aliponda suala la viwanja kuwa na sehemu za watu kusimama badala ya wote kukaa chini kwani suala hilo linahatarisha usalama wa watazamaji haswa wanaokwenda uwanjani na familia zao.

No comments:

Post a Comment