Thursday, August 23, 2012

WIZARA MISRI KUANZA KUWARUHUSU MASHABIKI.

WIZARA ya Mambo ya Ndani nchini Misri inatarajiwa kuwaruhusu baadhi ya mashabiki wa soka nchini humo kuhudhuria baadhi ya mechi ikiwa kama sehemu ya majiribio kwa wizara hiyo. Wizara hiyo inatarajiwa kuwaruhusu mashabiki kuhudhuria baadhi ya michezo ikiwemo mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Zamalek na Chelsea Berekum . Taarifa kutoka katika wizara hiyo inaendelea kusema kuwa michezo ambayo inawakutanisha timu mahasimu bado mashabiki wataendelea kuzuiwa ikiwemo mchezo wa mzunguko wa mwisho wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Al Ahly na Zamalek. Mechi zote zilizochezwa nchini Misri katika kipindi cha miezi sita iliyopita zilichezwa bila ya mashabiki baada ya wizara kuzuia kutokana na vurugu zilizotokea jijini Port Said. Zamalek itamenyana na Chelsea ya Ghana mwezi ujao katika michuano hiyo wakati Al Ahly itasafiri kwenda Lubumbashi ambapo watakutana na TP Mazembe katika mchezo ambao unatarajiwa kuwa mkali.

No comments:

Post a Comment