Thursday, August 23, 2012

CRUYFF AMPONDA MOURINHO KUJIITA "THE ONLY ONE".

NYOTA wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi na klabu ya Barcelona Johan Cruyff amemtaja meneja wa Real Madrid Jose Mourinho kama mtu ambaye alifeli akiwa kama mchezaji. Cruyff alitoa kauli hiyo kwa kucheka baada ya Mourinho ambaye ni raia wa Ureno kujipachika jina la “the only one” akimaanisha kwamba ni yeye pekee. Akihojiwa kuhusiana na kauli hiyo ya Mourinho Cruyff amesema kuwa si kweli Mourinho kafanya mambo makubwa mpaka ajiite hivyo kwasababu hakuwa na chochote cha kujisifu wakati akiwa mchezaji. Mbali na kumshabulia Mourinho, nyota huyo wa zamani pia alimponda rais wa Barcelona Sandro Rosell kuhusu sera za uhamisho wa klabu yake hiyo ya zamani kuwa zinahitaji marekebisho. Cruyff amesema kuwa sera nzuri ni kutengeneza wachezaji na sio kununua kama anavyofanya Rosell ambapo hivi karibuni alimnunua Alex Song kutoka Arsenal ili aje kuongeza nguvu katika klabu hiyo. Cruyff pia amesema kocha wa sasa wa klabu hiyo Tito Vilanova ana kazi kubwa ya kufanya ili kufikia mafanikio aliyopata Pep Guardiola wakati akiinoa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment