Thursday, August 23, 2012

SCHMEICHEL KUHUDHURIA FAINALI YA AIRTEL RISING STARS NAIROBI.

GOLIKIPA nyota wa zamani wa kimataifa wa Denmark na klabu ya Manchester United, Peter Schmeichel anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika fainali ya michuano ya Airtel Rising Stars itakayofanyika Jumamosi jijini Nairobi, Kenya. Katika shughuli hiyo Schmeichel atapata nafasi ya kutaja majina katika orodha ya wachezaji ambao wamechaguliwa kwenda kuweka kambi katika klabu za Arsenal na Manchester United nchini Uingereza. Makamu wa rais wa Airtel Afrika Achieng Butler alidokeza sababu kubwa ya kumleta nyota huyo nchini humo ni kuwapa vijana motisha na uchu wa kufikia mafanikio katika maisha yao ya soka. Michuano hiyo ya Airtel Afrika ilifunguliwa rasmi Jumatatu na Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga katika Uwanja wa Jiji uliopo Nairobi na fainali inatarajiwa kuchezwa katika uwanja huohuo.

No comments:

Post a Comment