Tuesday, September 25, 2012

ILIKUWA NIJIUNGE NA TOTTENHAM - HAZARD.

NYOTA wa klabu ya Chelsea Eden Hazard ameweka wazi kuwa alikuwa ajiunge na klabu ya Tottenham Hotspurs lakini alibadilisha mawazo baada ya klabu hiyo kushindwa kufuzu michuano ya Ligi ya mabingwa Ulaya. Hazard pia alikataa nafasi ya kujiunga na klabu za Manchester United na Manchester City kabla ya kukubali kujiunga na Chelsea akitokea Lille kwa ada ya paundi milioni 32. Akizungumza kwa mara ya kwanza kuhusiana na sakata la uhamisho wake ambao ulizua mjadala katika kipindi hicho Hazard amesema kuwa aliyekuwa meneja wa Tottenham Harry Redknapp alimfuata kumsajili ili akazibe pengo la Luka Modric. Nyota huyo anasema kuwa katika kipindi hicho ambapo Spurs ilikuwa katika nafasi ya tatu alishawishika kujiunga na klabu hiyo lakini ilipokosa nafasi ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa alibadilisha mawazo na kuangalia ofa za klabu nyingine.

No comments:

Post a Comment