Tuesday, September 25, 2012

WALCOTT ATAMANI KUVAA VIATU VYA HENRY.

MSHAMBULIAJI nyota wa pembeni wa klabu ya Arsenal, Theo Walcott amesema kuwa nataka kubakia klabuni hapo na kuwa nguli wa klabu hiyo kama ilivyokuwa kwa mshambuliaji nyota wa klabu hiyo yenye maskani yake Kaskazini mwa jiji la London Thierry Henry. Nyota huyo alikanusha tuhuma kuwa kuchelewa kwake kusaini mkataba mpya kunahusiana na suala la fedha lakini alikubali kuwa suala ya kusaini mkataba mwingine litachukua muda. Meneja wa klabu ya Arsenal alionya wiki iliyopita kuwa wanaweza kulazimika kumuuza mchezaji huyo kitu ambapo kilikaribia kutokea msimu uliopita kama hawatafikia makubaliano pindi dirisha la usajili likifunguliwa tena. Walcott amekuwa akitaka kuhakikishiwa kupata namba muda wote katika kikosi cha Wenger na apangwe kama mshambuliaji wa kati. Wenger alimuondoa Henry ambaye alikuwa anacheza kama winga na kuja kuwa mshambuliaji anayeongoza kwa mabao katika historia ya klabu hiyo na Walcott ambaye ndiye amerithi jezi namba 14 aliyokuwa akivaa nguli naye aje kufikia mafanikio yake.

No comments:

Post a Comment