Thursday, September 20, 2012

MAOFISA WA SOKA CAMEROON KUMWANGUKIA ETO'O.

MAOFISA wa soka nchini Cameroon wamegawanyika juu ya ujumbe ambao utasafiri kuelekea nchini Urusi kujaribu kuongea na mshambuliaji nyota na nahodha wa zamani wan chi hiyo Samuel Eto’o kujaribu kubadilisha uamuzi wake wa kuachana na soka la kimataifa. Kufuatia kuteuliwa kwake kuziba nafasi ya aliyekuwa kocha wan chi hiyo Denisi Lavagne, Jean Paul Akono ameweka suala ya kumrejesha mchezaji huyo kama jukumu lake la kwanza kabla timu hiyo haijakabiliwa na mchezo wa pili wa kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Cape Verde Octoba 13 mwaka huu. Kumekuwa na msuguano wa chini kwa chini kwakuwa baadhi ya maofisa wa wizara ya michezo ya nchi pamoja na wale wa soka wamekuwa wakipinga suala hilo la kwenda kumwangukia mchezaji huyo ili arejee kuitumikia Cameroon. Cameroon iko katika hatari ya kushindwa kufuzu michuano hiyo baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Cape Verde katika mchezo wa kwanza uliofanyika jijini Praia lakini kabla ya hapo Eto’o alijitoa katika timu hiyo kwa kile alichodai uongozi mbovu wa soka nchini humo.

No comments:

Post a Comment