Thursday, September 20, 2012

SHAKIRA, PIQUE WATEGEMEA MTOTO.

MWANAMUZIKI nyota kutoka Colombia, Shakira amesema kuwa anategemea kupata mtoto wa kwanza na mpenzi wake ambaye ni mcheza soka wa kimataifa wa Hispania, Gerard Pique. Shakira mwenye umri wa miaka 35 aliandika katika mtandao wake kuwa yeye pamoja na Pique wako katika kilele cha furaha wakisubiria kuzaliwa kwa mtoto wao wa kwanza na hilo ndio jambo pekee ambalo wanalitilia mkazo kwasasa. Mapema wiki hii mwanamuziki huyo pamoja na nyota mwingine wa R&B Usher Raymond walithibitishwa kuziba nafasi za Christina Aguilera na Cee Lo Green katika msimu wa nne wa mashindano ya kuimba yanayoandaliwa na NBC yanaoitwa The Voice. Shakira alianza kujulikana kimataifa katika muziki wa pop baada ya kuipua wimbo wake uliotamba mwaka 2006 unaoitwa Hips Don’t Lie na alikutana na Pique mwenye umri wa miaka 25 katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2010 nchini Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment