Wednesday, September 26, 2012

MUSONYE AMPONDA KOCHA WA HARAMBEE STARS.

KATIBU Mkuu wa Baraza la Michezo kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati-CECAFA, Nicholas Musonye amemjia juu kocha wa timu ya taifa ya Kenya-Harambee Stars Henry Michel kwa kauli yake kuhusiana na michuano ya Kombe la Challenge. Musonye amejia juu Michel kufuatia kauli yake aliyotoa kuwa anaipa umuhimu wa kwanza mechi za kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani-CHAN tofauti na michuano hiyo ya CECAFA. Akihojiwa kuhusiana na kauli aliyotoa Michel, Musonye amesema kuwa hakuna chochote cha maana kocha huyo alichofanya katika kuendeleza soka la Afrika na kama yeye ndiye angetakiwa kumwajiri asingefanya hivyo. Musonye aliendelea kusema kuwa kocha huyo angetimiza wajibu wake katika timu hiyo na sio kujiingiza katika siasa ambazo zimetawala kwenye Shirikisho la Soka nchini Kenya-FKF. Mara ya mwisho Kenya kunyakuwa Kombe la CECAFA ilikuwa mwaka 2002 ambapo Dennis Oliech alifunga bao la ushindi kwa timu hiyo dhidi ya Tanzania-Taifa Stars katika fainali ambayo walishinda mabao 3-2.

No comments:

Post a Comment