Wednesday, September 26, 2012

SCOLARI APEWA SHAVU BRAZIL.

LUIZ Felipe Scolari ambaye aliiwezesha Brazil kunyakuwa taji lake la tano la Kombe la Dunia mwaka 2002 akiwa kocha wa timu hiyo amesema kuwa anatarajia kuanza tena kazi ukocha mwaka 2013. Kocha huyo anayejulikana kwa misimamo isiyopinda amesema kuwa anatarajiwa kupata kibarua mwakani lakini hajaweka wazi kama itakuwa akinoa timu za taifa au klabu ingawa huko nyuma amesema kuwa anatamani awe kocha wa timu yoyote ya taifa katika Kombe la Dunia mwaka 2014 litakalofanyika Brazil. Scolari ambaye mbali na kuipa Brazil Kombe la Dunia mwaka 2002 pia ameiwezesha klabu ya Palmeiras ya nchi hiyo kunyakuwa ubingwa taifa mara nane klabu ya kubwaga manyanga wiki mbili zilizopita kwasababu ya kushindwa kuitoa timu hiyo katika mstari wa kushuka daraja. Kauli hiyo ya Scolari aliitoa jana wakati Waziri wa Michezo wa Brazil akimtangaza kocha huyo kufanya kazi mshauri ambaye atakuwa akiwahubiria vijana uzoefu wake katika mchezo wa soka na kutangaza Kombe la Dunia.

No comments:

Post a Comment