Wednesday, September 26, 2012

CHELSEA YAMTENGEA FALCAO KITITA CHA PAUNDI MILIONI 45.

KLABU ya Chelsea imepanga kutenga kitita cha paundi milioni 45 ili kumnasa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Colombia Radamel Falcao. Mazungumzo ya kwanza juu ya uhamisho wa mchezaji huyo kutoka Atletico Madrid katika kipindi cha dirisha dogo la usajili Januari mwakani tayari yameshaanza na mmiliki wa Chelsea Roman Abramovic tayari amemtengea pesa mchezaji huyo ambaye aliisambaratisha timu hiyo katika michuano ya Super Cup. Chelsea ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya wanaamini kuwa itakuwa ngumu kwao kutetea taji hilo kama watakuwa wakimtegemea mshambuliaji mmoja ambaye ni Fernando Torres. Falcao mwenye umri wa miaka 26 tayari amefunga mabao 115 katika kipindi cha miaka mitatu ambacho amecheza soka Ulaya yakiwemo mabao matatu aliyoifunga Chelsea katika fainali ya Super Cup iliyofanyika jijini Monaco.

No comments:

Post a Comment