Wednesday, September 26, 2012

BOND AFARIKI DUNIA.

MENEJA wa zamani wa klabu za Norwich na Manchester City za Uingereza, John Bond amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 79. Katika kipindi cha miaka mitatu ambayo alikuwa akiinoa City, Bond aliiwezesha klabu hiyo kutinga fainali ya Kombe la FA mwaka 1981 lakini alipoteza mchezo wa fainali kwa Tottenham Hotspurs. Mbali na kuifikisha City katika fainali ya FA, Bond pia aliiwezesha Norwich kutinga fainali ya ya Kombe la Ligi mwaka 1975 ambapo walipoteza mchezo huo kwa klabu ya Aston Villa kwa kufungwa bao 1-0. Mbali na kuzinoa klabu hizo Bond aliwahi kucheza katika klabu ya West Ham kwa kipindi cha miaka 16 akiwa amecheza michezo 144 na kuisaidia timu hiyo kushinda Kombe la FA mwaka 1964.

No comments:

Post a Comment