Sunday, September 30, 2012

MWAMUZI ALITUPUNJA MUDA WA NYONGEZA - FERGUSON.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson amesema kuwa muda wa dakika nne za nyongeza alizotoa mwamuzi wakati timu yake ikifungwa Tottenham Hotspurs hazikuwa sahihi. Clint Dempsey ndiye aliyefunga bao la ushindi na kuifanya Spurs kutoka na ushindi wa mabao 3-2 katika Uwanja wa Old Traford kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 23. Ferguson amesema kuwa dakika nne za nyongeza zilizotolewa na mwamuzi zilikuwa chache kutokana na Spurs kupoteza dakika nyingi katika mchezo huo. Kocha huyo aliendelea kusema kuwa ni kitu kinachokatisha tamaa kwasababu walikuwa na rekodi nzuri lakini anadhani mwamuzi alichangia kuwafanya wapoteze mchezo huo baada ya kuongeza muda mchache kulinganisha na ule ambao wapinzani walikuwa wakipoteza katika dakika 90. Hicho kinakuwa kipigo cha pili kwa United katika michezo sita ya Ligi Kuu nchini Uingereza waliyocheza msimu huu ambapo sasa wanashika nafasi ya tatu nyuma ya vinara wa ligi hiyo Chelsea na Everton.

No comments:

Post a Comment