Sunday, September 30, 2012

NILIPANGA KUMPUMZISHA TERRY - DI MATTEO.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Roberto di Matteo amekiri kuwa alitaka kumuondoa John Terry katika kikosi chake ambacho kiliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Arsenal katika Uwanja wa Emirates jana. Terry alijumuishwa katika kikosi hicho ikiwa ni siku mbili toka alipofungiwa mechi nne na kutozwa faini ya paundi 220,000 na Chama cha Soka nchini Uingereza-FA baada ya kukutwa na hatia ya kumfanyia ubaguzi wa rangi beki wa Queens Park Rangers, Anton Ferdinand. Adhabu imekuja kufuatia tukio baina ya timu hizo ambazo ni mahasimu wa Magharibi mwa jiji la London Octoba mwaka jana ingawa hatahivyo adhabu itaanza pale ambapo muda wa kukata rufani utakapokwisha. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Di Matteo ambaye ni kiungo wa zamani wa kimataifa wa Italia na Chelsea amesema kuwa alifikiri kumuacha nahodha wake huyo katika mchezo huo lakini uamuzi wa kumjumuisha ulikuwa mzuri kutoka kiwango bora alichoonyesha.

No comments:

Post a Comment