Sunday, September 30, 2012

RONALDO ATAMANI KUWA MCHEZAJI ANAYELIPWA ZAIDI DUNIANI.

TAMAA ya mshambuliaji nyota wa klabu ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo kuwa mchezaji anayelipwa zaidi duniani kunaongeza kukua kwa mgawanyiko ndani ya klabu hiyo kitendo ambacho kinavistua vilabu vingine tajiri barani Ulaya. Mmiliki wa klabu ya Chelsea pamoja na tajiri wa kiarabu anayemiliki Manchester City na klabu ya Paris saint-Germain ya Ufaransa ndio wanaoongoza katika orodha ya timu ambazo zinawinda saini ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 27. Mshahara wa Ronaldo wa Euro milioni 7.98 ambao ni nusu na mshahara anaopata Samuel Eto’o katika klabu ya Anzi ya Urusi unamfanya nyota huyo kuwa wa 10 miongoni mwa orodha ya wachezaji wanaolipwa zaidi duniani. Nyota alikuwa akihitaji nyongeza ya asilimia 50 katika mshahara wake lakini suala hilo litakuwa gumu katika klabu hiyo kutokana na hali mtikisiko wa kiuchumi ulioikumba nchi hiyo katika kipindi cha hivi karibuni. Mapema mwezi huu Ronaldo alihojiwa na kudai kuwa suala la kitaaluma ndilo linalomsababisha akose furaha na klabu hiyo inajua hilo kauli ambayo ilizua mijadala katika vyombo mbalimbali vya habari duniani juu ya mstakabali wa mbeleni wa nyota huyo.

No comments:

Post a Comment