Sunday, September 30, 2012

URUSI YATANGAZA MIJI ITAKAYOTUMIKA KOMBE LA DUNIA.

NCHI ya Urusi imetangaza miji 11 ambayo itakuwa wenyeji wa michuano ya Kombe la Dunia 2018 ikiwa ni mradi wa kwanza mkubwa kufanywa na nchi toka kuanguka kwa iliyokuwa USSR. Michuano hiyo mikubwa kabisa duniani itachezwa katika miji ya Moscow, Saint Petersburg, Sochi mji ambao pia uwakuwa mwenyeji wa michuano ya Olimpiki ya kipindi cha baridi 2014, Kazan, Yekaterinburg, Kaliningrad, Nizhny Novgorod, Samara, Rostov-on-Don, Saransk na Volgograd. Katika sherehe hizo zilizokuwa zikionyeshwa moja kwa moja katika luninga, huku zikiongozwa na Rais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Sepp Blatter na Waziri wa Michezo wa nchi hiyo Vitaly Mutkoongozwa miji miwili ya Yaroslavl na Krasnodar iliondolewa katika orodha iliyokuwa na miji 13. Tofauti na michuano ya Olimpiki ya kipindi cha baridi, Kombe la Dunia litaihitaji serikali kutumia mabilioni ya dola kwa ajili kuendeleza viwanja, utalii na miundo mbinu ya usafiri kwa nchi nzima. Urusi ilipewa nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia 2018 katika uchaguzi uliogubikwa na utata Desemba mwaka 2010 ambapo ulishuhudia nchi ya Qatar nayo ikipewa nafasi ya kuandaa michuano 2022 kwa kuishinda Uingereza ambayo nayo ilikuwa inataka nafasi hiyo.

No comments:

Post a Comment