Wednesday, November 21, 2012

DI MATTEO ATIMULIWA CHELSEA.

Mabingwa wa Ulaya klabu ya Chelsea imeamua rasmi kuvunja mkataba na kocha wake Roberto Di Matteo kufuatia matokeo mabaya ambayo yamekuwa yakiikabili timu hiyo katika michezo yake ya hivi karibuni. Hatua ya klabu hiyo kumtimua Di Matteo imekuja kufuatia kufungwa na Juventus kwa mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kipigo ambacho kimewaweka katika hati hati ya kushindwa kusonga mbele katika michuano hiyo. Katika taarifa iliyotumwa katika wavuti wa klabu hiyo imesema kuwa klabu hiyo imeamua kufanya mabadiliko ya haraka baada ya kuona timu hiyo kisuasua katika michiano mbali mbali inayoshiriki ikiwemo ligi ya mabingwa na ligi kuu nchini Uingereza. Taarifa iliendelea kusema kuwa klabu itatangaza muda mfupi baadae meneja ambaye atachukua mikoba ya Di Matteo. 




No comments:

Post a Comment