Wednesday, November 21, 2012

EUROPA LEAGUE ACTION.

Michuano ya Ligi ya Ulaya maarufu kama Europa League inatarajiwa kutimua vumbi tena leo huku kila timu ikijaribu kuhakikisha inatinga katika hatua ya timu 32 bora za michuano hiyo. Timu za Anzhi mkhachkala ya Urusi, Udinese ya Italia, Liverpool ya Uingereza na Young Boys ya Switzerland zote zitajitupa uwanjani kusaka ushindi ili kujihakikishia nafasi ya kusonga mbele katika michuano hiyo. Katika michezo mingine ya leo mabingwa watetezi wa michuano hiyo Atletico Madrid ya Hispania itaikaribisha Hapoel Tel Aviv ya Israel, Rubin Kazan ya Urusi nao watakuwa wenyeji wa Inter Milan ya Italia wakati Basel ya Swtzerland itaikaribisha Sporting Lisbon ya Ureno. Katika viwanja vingine Tottenham Hotspurs watakuwa na kibarua kigumu cha kusaka ushindi ugenini mbele ya Lazio ya Italia wakati waingereza wenzao Newcastle United wenyewe watakuwa nyumbani kuikabili Maritimor ya Ureno.

No comments:

Post a Comment