Thursday, November 29, 2012

FERRARI CONSIDER SEBASTIAN VETTEL PROTEST.

TIMU ya Ferrari inajaribu kuangalia kama kuna ushahidi wa kutosha ili waweze kupinga matokeo ya ubingwa wa dunia wa mashindano ya Langalanga na wakifanikiwa kuna uwezekano mkubwa matokeo hayo yakabadilishwa. Timu hiyo inafuatilia picha za video ambazo zinamuonyesha dereva wa Red Bull Sebastian Vettel akilipita gari lingine kimamkosa katika mashindano ya Grand Prix iliyofanyika nchini Brazil Jumapili iliyopita. Fernando Alonso kutoka Hispania alipoteza taji hilo kwa alama toka kwa Vettel lakini mjerumani huyo anaweza kupoteza alama nne kama akikutwa na hatia ya kuvunja sheria katika mashindano hayo. Chombo cha Kusimamia mashindano hayo-FIA kimekataa kuthibisha kama kinafanyia uchunguzi tukio hilo. Picha za video zinamuonyesha Vettel akimpita dereva wa timu ya Toro Rosso, Jean Eric mahali ambapo haparuhusiwi katika mzunguko wa nne wa michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment