Thursday, November 29, 2012

MANCINI AMPONDA BALOTELLI.

MENEJA wa klabu ya Manchester City, Roberto Mancini amesema bado hajafurahishwa na kiwango cha mshambuliaji wa timu hiyo Mario Balotelli pamoja na nyota huyo kufunga bao lake la kwanza la Ligi Kuu msimu huu dhidi ya Wigan Athletic jana usiku. Balotelli ambaye ameanza katika kikosi cha kwanza mara sita kati ya 14 msimu huu alifunga bao la kuongoza dakika ya 69 wakati Cit ambao hawajapoteza mchezo wa ligi msimu huu wakishinda mabao 2-0 na kubakia nafasi ya pili katika msimamo nyuma ya Manchester United kwa tofauti ya alama moja. Mancini alimsifisia mshambuliaji huyo kwa kufunga bao muhimu katika mchezo huo lakini kocha anafikiri kuwa Balotelli anaweza kufanya vizuri zaidi ya hapo kwasababu ni mchezaji wa kiwango cha juu. Kocha aliendelea kusema kuwa kama mchezaji huyo akiongeza bidii katika mazoezi anaweza kufikia kiwango cha Cristiano Ronaldo au Lionel Messi.

No comments:

Post a Comment