Thursday, November 29, 2012

SCOLARI ATAJWA KUCHUKUA MIKOBA YA MENEZES.

Kuna habari zimesambaa nchini Brazil kuwa Luiz Felipe Scolari ndio anatarajiwa kuwa mpya wa timuya taifa ya nchi hiyo. Brazil imekuwa katika mchakato wa kutafuta kocha mpya baada ya kumtimua Mano Menezes Ijumaa iliyopita kufuatia kushindwa kufikia malengo waliyoweka katika michuano ya Olimpiki iliyofanyika jijini London mwaka huu. Scolari ambaye alikiongoza kikosi cha Brazil kunyakuwa Kombe la Dunia mwaka 2002 amekuwa hana kibarua kwasasa baada ya kuondoka katika klabu ya Palmeiras Septemba mwaka huu. Taarifa hizo zilisema kuwa Scolari ambaye amewahi kukinoa kikosi cha Chelsea alifanya mazungumzo na viongozi wa Shirikisho la Soka nchini Brazil-CBF ambapo anatarajiwa kutangazwa rasmi baadae. Rais wa CBF Jose Maria Marin alithibitisha kufanya mazungumzo na makocha kadhaa ingawa hakutaja jina la Scolari ili kuangalia ni kocha gani wanaweza kumpa mikoba ya kuingoza Brazil katika michuano ya Kombela Dunia 2014 ambayo wao watakuwa wenyeji.

No comments:

Post a Comment