Wednesday, November 28, 2012

CASILLAS AWAPONDA MASHABIKI WANAOMZOMEA MOURINHO.

NAHODHA wa klabu ya Real Madrid, Iker Casillas amemkingia kifua Jose Mourinho baada ya kocha huyo raia wa Ureno kupigiwa filimbi na baadhi ya mashabiki wa timu hiyo wakati wa mchezo wa Kombe la Mfalmeuliofanyika katika Uwanja wa Santiago Bernabeu Jumanne. Kumekuwa na shinikizo la mgawanyiko kuhusu Mourinho baada ya kikosi chake kuwa nyuma kwa alama 11 mbele ya mahasimu wao Barcelona ambao wanaongoza La Liga ndio sababu kubwa iliyochangia mashabiki hao kupiga filimbi huku wengine wakitaja jina lake katika mchezo huo ambao Madrid ilishinda mabao 3-0 dhidi ya Alcoyano. Casillas amesema kuwa anadhani miezi michache iliyopita watu ambao walikuwa wakipiga filimbi katika mchezo wa Jumanne ndio watu ambapo walikuwa wakipiga makofi na kushangilia wakati waliposhinda taji la La Liga. Kipa huyo aliongeza kuwa kumbukumbu huwa ni ndogo katika soka na labda watu wamesahau ni nani aliyekiongoza kikosi cha timu hiyo kushinda taji la La Liga kwa kuweka rekodi ya kufunga mabao mengi na kupata alama nyingi zaidi. Aliendelea kusema kuwa mashabiki wanatakiwa kukumbuka na nyakati za furaha ambazo walipata na kuendelea kuishangilia timu yao ili iweze kufanya vizuri zaidi.

No comments:

Post a Comment