Wednesday, November 28, 2012

MSAIDIZI WA MANCINI AFUNGIWA MECHI MBILI NA UEFA.

SHIRIKISHO la Soka la Ulaya-UEFA limemfungia mechi mbili za Ulaya kocha msaidizi wa Manchester City, David Platt baada ya kutolewa na kupelekwa jukwaani wakati wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid wiki iliyopita. Platt hataruhusiwa kuwepo katika benchi la wachezaji wa akiba wakati wa mchezo wa mwisho wa City dhidi ya Borussia Dortmund wiki ijayo. Katika taaifa ya UEFA`ambayo ilitumwa katika wavuti wake imesema kuwa Kamati ya Nidhamu ilimkuta na kosa Platt kwakuonyesha tabia isiyofaa katika mchezo huo hivyo kupelekea mwamuzi kumwamuru kwenda kukaa jukwaani. UEFA pia imeitoza faini ya paundi 12,000 klabu ya Manchester City baada ya wachezaji wake watano kupewa kadi za katika mchezo huo ambapo wamepewa siku tatu kama wanataka kukata rufani kuhusiana na adhabu hizo.

No comments:

Post a Comment