Wednesday, November 28, 2012

UEFA YAFIKIRIA KUONGEZA TIMU 32 ZAIDI LIGI YA MABINGWA ULAYA.

SHIRIKISHO la Soka barani Ulaya-UEFA linafikiria kuikacha michuano ya Europa League ili kuboresha michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuongeza timu zaidi kutoka 32 mpaka tinu 64. Rais wa UEFA, Michel Platini amesema kuwa bado wako katika mazungumzo na wanatarajia kutoa maamuzi 2014 kwasasa hakuna lolote lililoamuliwa kuhusiana na suala hilo. Kama mabadiliko hyo yakipitishwa inamaanisha Uingereza itakuwa na saba katika hatua ya makundi ya michuano hiyo, nne ambazo huyo zinafuzu ligi ya mabingwa na tatu zingine zinazoshiriki Europa League. UEFA inapanga kubadilisha mfumo wa mashindano ya Ulaya kuanzia mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment