Tuesday, November 20, 2012

HENRY KUREJEA TENA ARSENAL JANUARI.

MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Arsenal, Thierry Henry anaweza kurejea tena katika klabu hiyo yenye maskani yake kaskazini mwa jiji la London kwa mkopo kutokea katika klabu ya New York Red Bull ya Marekani Januari mwaka huu. Meneja wa Arsenal, Arsenal Wenger alibainisha hayo katika wavuti wa klabu hiyo kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kumsajili nyota huyo katika kipindi cha dirisha dogo la usajili kwasababu amekuwa akifanya nao mazoezi nab ado anaonekana ana uwezo ya kukabiliana na mikiki ya ligi. Henry ambaye ana rekodi ya kufunga mabao 228 alirejea katika klabu hiyo Januari mwaka jana na kufunga bao katika mchezo dhidi ya Leeds United katika Kombe la FA na kufunga bao la ushindi katika dakika za mwisho katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Uingereza dhidi ya Sunderland. Wenger ameonyesha nia ya kumrejesha tena shujaa wake huyo na anaamini kuwa anaweza kuwa msaada mkubwa haswa ikizingatiwa kuwa anaweza kuwapoteza washambuliaji wake wawili Gervinho kutoka Ivory Coast na Marouane Chamakh ambao kuna uwezekano mkubwa wa kuitwa kuzitumikia timu zao za taifa katika Kombe la Mataifa ya Afrika Januari mwakani. 

No comments:

Post a Comment