Tuesday, November 20, 2012

MESSI AENDELEA KUVUNJA REKODI MBALIMBALI.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Lionel Messi ameendeleza rekodi yake ya kufunga mabao baada ya kufunga mabao mawili katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya ambao timu yake ilishinda mabao 3-0 dhidi ya Spartak Moscow. Mabao hayo ya nyota huyo aliyofunga jana yamemwezesha kufikisha mabao 56 katika michuano hiyo ya Ulaya na kumuweka sawa katika nafasi ya pili ya wafungaji bora wa bara hilo akiwa sambamba na Ruud van Nisterlrooy wakizidiwa na Raul ambaye yeye amefunga mabao 71. Messi pia amefikia rekodi ya Raul ya kufunga bao katika nchi 19 tofauti katika michuano ya Ligi ya Mabingwa na kumpita nyota huyo huyo wa zamani kwa kufunga mabao zaidi ya mawili katika mechi 14 za michuano hiyo. Nyota huyo amebakisha mabao matano pekee kufikia rekodi ya Gerd Muelller aliyefunga mabao 85 ndani ya mwaka mmoja katika mashindano yote rekodi ambayo aliiweka mwaka 1972. Messi amekuwa akiongoza kwa kufunga mabao mengi zaidi katika Ligi ya Mabingwa Ulaya katika kipindi cha miaka minne iliyopita huku msimu uliopita akifikisha mabao 14 ambayo ndio mengi zaidi kwa msimu.

No comments:

Post a Comment