Wednesday, November 21, 2012

BOLT KUHAMIA KATIKA KRIKETI AU SOKA BAADA YA 2016.

Mwanariadha nyota wa mbio fupi USAIN BOLT anatarajiwa kutoshiriki mashindano ya riadha ambayo ni ya mwisho kwa mwaka huu ya Twenty20 League lakini ataweza kuhamia katika mchezo wa kriketi au soka baada ya michuano ya Olimpiki 2016. Wakala wa mwanariadha huyo RICKY SIMMS amesema kuwa kwasasa nyota huyo ni mwanariadha alielekeza nguvu zake katika maandalizi ya mashindano ya Dunia ya riadha yatakayofanyika jijini Moscow 2013. SIMMS alikiri kuwa nyota huyo ana ndoto za kucheza kriketi au soka wakati ambapo atastaafu mchezo wa riadha lakini itakuwa baada ya olimpiki ya 2016 itakayofanyika jijini Reo de Janeiro, Brazil. BOLT ni mwanariadha anayepewa heshima kubwa kwasasa baada ya kufanikiwa kutetea mataji yake yam bio za mita 100, 200 na mita 400 za kupokezana vijiti katika michuano ya olimpiki iliyofanyika iliyopita.

No comments:

Post a Comment