Tuesday, November 20, 2012

JUVENTUS YAMUWINDA DROGBA.

KLABU ya Juventus ya Italia inapanga kumsajili mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Ivory Coast Didier Drogba anayecheza kwenye klabu ya Shanghai Shenhua ya China katika kipindi cha dirisha dogo la usajili Januari mwakani. Mabingwa hao wa Serie A wamekuwa sokoni kwa kipindi kirefu wakitafuta mshambuliaji ambapo katika kipindi cha karibuni wamekuwa wakihusishwa na Fernando Llorente na Pablo Asvaldo na hivi sasa wamehamishia nguvu zao kumsajili Drogba mwenye umri wa miaka 34. Drogba alijunga na kabu hiyo inayoshiriki Ligi kuu nchini China kutoka Chelsea katika kipindi cha usajili cha majira ya kiangazi lakini anaonekana hana furaha na ana nia ya kurejea Ulaya tena. Sababu ya Drogba ambaye analipwa euro milioni 12 kwa mwaka ni kutofurahishwa na mazingira ya klabu hiyo kumcheleweshea mshahara wake zaidi ya mara moja toka alipohamia huko. Hatahivyo Juventus wanakabiliwa na wakati mgumu wa kumsajili mchezaji huyo kwa kuwa wamepanga kupunguza mshahara wake kama akikubalia kujiunga nao na kumlipa euro milioni 4.5 kwa mwaka pamoja na posho nyingine.

No comments:

Post a Comment