Tuesday, November 20, 2012

HUGHES KUBAKIA QPR.

MENEJA wa Queens Park Rangers, Mark Hughes atabakia kuinoa klabu hiyo ambayo inasuasua katika mstari wa kushuka daraja kufuatia mkutano aliofanya na Ofisa Mkuu wa klabu hiyo Philip Beard. Kuna taarifa zilizosambaa kuwa Hughes ambaye amewahi kuwa kocha wa Wales alifukuzwa baada ya wawili kukutana katika uwanja wa mazoezi jana lakini mwakilishi wa kocha huyo Kia Joobchian alikanusha tetesi hizo na kudai sio za kweli. Hughes amekuwa na matokeo mabaya toka mwanzoni mwa msimu huu akiwa ameambulia alama nne pekee katika michezo 12 ambayo timu hiyo imecheza msimu huu hivyo kushika mkia katika msimamo wa Ligi Kuu nchini Uingereza. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 49 ambaye amewahi kuzifundisha klabu za Blackburn Rovers, Manchester City na Fulham amesisitiza kuwa hawezi kujiuzulu kibarua hicho kufuatia kufungwa nyumbani mabao 3-1 na Southampton ambao wote wanapigania kutoshuka daraja.

No comments:

Post a Comment