Tuesday, November 20, 2012

KAGAWA KUKAA NJE WIKI NNE ZAIDI.

KIUNGO nyota wa klabu ya Manchester United, Shinji Kagawa ameongezewa wiki zingine nne kukaa nje ya uwanja kutokana na majeruhi yanayomsumbua. Kiungo huyo wa kimataifa wa Japan mwenye umri wa miaka 23 aliumia mguu wakati wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya ambao timu yake ilishinda kwa mabao 3-2 dhidi ya Braga Oktoba 23 mwaka huu. Meneja wa United Sir Alex Ferguson alimtegemea mchezaji huyo kupona katika kipindi cha wiki nne mpaka tano lakini nyota huyo ameonekana kupona taratibu hivyo kuna uwezekano wa kukaa nje ya uwanja kwa nyingine nne nyingine. Pamoja na habari mbaya kuhusu Kagawa lakini Ferguson amefarijika baada ya beki wake nyota Phil Jones kurejea katika kikosi chake baada ya kuumia mgongo wakati maandalizi ya msimu mpya wa ligi hiyo. Beki huyo mwenye umri wa miaka 20 anatarajiwa kuwepo katika mchezo wa kundi H leo ambapo United watakuwa wageni wa Galatasaray ya Uturuki.

No comments:

Post a Comment